TED WILSON AWATAKA VIONGOZI WA KANISA WASIO NA IMANI JUU YA BIBLIA KUJIUZULU - OKTOBA 7, 2023
Na Gerry Wagoner
Ukosefu wa ufahamu wa Biblia* jinsi ya kuifasiri na uadui dhidi
ya Neno la Mungu. Kanisa la SDA linaamini katika uhalisi na mamlaka ya Biblia
Takatifu na inapaswa kutumika kwa watu wote kila mahali, kwa wakati wote.
Kanisa linakubali tu mbinu ya kihistoria ya kibiblia au ya kihistoria ya
kisarufi ya kufasiri Maandiko, ikiruhusu Biblia kujitafsiri yenyewe kwa nguvu
za Roho Mtakatifu. Nataka uiweke akilini mwako, tunashambuliwa na mbinu
nyingine za kufasiri Biblia. Mbinu hizo hazilengi kuleta utukufu kwa Mungu,
bali ni za kibinadamu. Hazikubaliki kwa Waadventista Wasabato. Ndani ya hizo,
mtu mwenyewe anakuwa mwamuzi wa kile ambacho ni kweli na kile ambacho sio
kweli. Ninawasihi tutumie mbinu ya wanahistoria pekee unapotafuta kuelewa
unabii wa Biblia. Sio mbinu ya MATUKIO YALIOKWISHA PITA, na sio ya MATUKIO
yajayo (Futurism). *_“Katika siku za mwisho, dunia itakuwa karibu kukosa imani
ya kweli” (SG 94)._* Usishawishiwe na watu katika kanisa la [SDA] wanaolidharau
Neno la Mungu.” Tunaikubali kama inavyosomwa!”
Baada ya mahubiri haya, wasaidizi wangu watapokea jumbe “Kwa
nini Wilson alisema hivyo?” Amekosea,” Tunaamini kwamba kuna Mungu [Uungu]
mmoja na Yeye anajumuisha Nafsi tatu za milele wanafanya kazi pamoja kwa umoja
Imani ya Msingi #2 ni wazi Mungu huyu wa utatu anataka kututumia ili kusaidia
kutekeleza mpango huu wa wokovu.
Mada nyeti. Tunapaswa kuonyesha heshima na kujali watu wote,
lakini Biblia iko WAZI juu ya maagizo ya Mungu kuhusu ngono ya binadamu. Biblia
iko wazi kwamba ndoa ni kati ya mwanamume mmoja TU na mwanamke [wa kibaolojia].
Kubadilika katika ujinsia wa mwanadamu HAUKUBALIWI na Mungu. Sio tu LGBTQ,
lakini pia uzinzi, uasherati, usagaji, ushoga, na mambo mengine yaliyo mbadala
wa ngono. Hizo ni dhambi. Kumbuka, sisi sote ni wenye dhambi chini ya msalaba.
Tunaposhughulika na hali hizi, shughulika kwa upendo, kwa staha na heshima,
lakini jua kile ambacho Biblia inasema hasa. Kwa bahati mbaya, baadhi ya watu
leo—hata ndani ya kanisa—tunafanya kazi na pande mbili na tawala zao ili
kukabiliana na changamoto za sasa katika eneo hili la [LGBTQ+]. Ngoja
nikuambie. Hakuna hata mmoja wetu katika migawanyiko yote ya ulimwengu ambaye
ana kinga dhidi ya hili. Watu wengine wanageuza Neno la Mungu, kama vile Warumi
1:18-32. Watu wengine wanatetea kwamba Warumi 1 inasema kile ambacho haisemi.
Soma Biblia kama inavyosomeka. Kanisa la ulimwenguni pote la SDA halikubali na
halitakubali watu binafsi kama washiriki wa kanisa au viongozi wa kanisa
waliochaguliwa ambao hawazingatii maagizo ya Biblia kuhusu ngono kwa binadamu.
Usikubali mtu yeyote anayetumia vibaya maagizo ya Biblia yanayopatikana katika
Warumi 1, Mambo ya Walawi 18, 20 na maandiko mengine mengi. Unaona, Neno la
Mungu linatuambia tusimame imara juu ya maagizo ya [Bwana] ametupa
uhakika kuhusu jambo hili na mambo mengine mengi. Kama ilivyo kwa mazoea
yoyote ya dhambi yaliyoainishwa katika Maandiko, tunapaswa kuwasaidia watu
wanaokuja kwenye makanisa yetu kupata msamaha kamili na maisha mapya chini ya
msalaba (2 Wakorintho 5:17). Tunaweza kufanywa viumbe vipya katika Yesu
[Amina].
Kuchanganyikiwa juu ya Huduma ya Patakatifu na Haki kwa Imani.*
Huduma ya patakatifu wa kidunia uliotolewa na Mungu kwa Musa ni
nakala ya moja kwa moja ya kile kilicho mbinguni. Inaonyesha mpango kamili wa
wokovu, kuonyesha upendo wa Mungu na dhabihu kuu ya Kristo. Huduma ya
patakatifu pa duniani na mbinguni ni funguo za kuelewa mchakato wa wokovu
unaojikita katika haki ya Yesu Kristo. SDA zinapaswa kuwa na makuu katika
kumwinua Yesu na haki yake. Usiruhusu mtu yeyote kusema kwamba sisi ni washika
sheria, tumejitoa kwa haki ya Kristo. Ni kiini hasa cha jumbe za malaika
watatu. Mnamo 1844 Kristo aliingia katika chumba cha pili cha patakatifu pa
mbinguni ili kuanza hukumu ya uchunguzi na sasa anafanya maombezi kama kuhani
wetu mkuu. Yeye ndiye njia yetu pekee ya uzima wa milele. Hatuokolewi kwa kuwa
WALA MBOGA. Nancy na mimi tujaribu kuwa wala mboga mboga na tumefaulu kwa
kiwango cha 95%. Hakika sisi ni walaji mboga, ambayo ni nzuri na wewe ninakupa
pia. Hatuokolewi kwa hilo. Hatuokolewi kwa zaka na sadaka zetu. Tunaokolewa kwa
neema na uwezo wa Yesu Kristo pekee.
Kanisa la SDA linaamini kwamba Mungu aliumba dunia hivi katika
siku sita halisi (kama zilivyi siku zetu). Mimi binafsi naamini kulingana na
Biblia na Roho ya Unabii kwamba dunia hii ina takriban miaka 6,000 tu. Sabato
ya siku ya saba ni ukumbusho wa tukio hilo la ajabu.
Wapo wengi. Baadhi yao hupunguza utakaso. Harakati moja ya
uwongo ambayo inazunguka vyuo vikuu vyetu na vyuo vikuu inaitwa Ukweli wa
Upendo. Ina mafundisho ya uongo kuhusu utakaso na kuhesabiwa haki. Imetoka
kwa-inapokelewa mara moja-kila wakati, ambapo SDA HATUAMINI HILO. Mungu
anakupenda kwa hivyo usijali kuhusu tabia yako ... Upendo wa Mungu una nguvu
sana lakini mafundisho haya ya uwongo ni hatari sana. Sikia hili. Kanisa la SDA
linapitia kipindi cha kupepetwa hivi sasa. Usijaribiwe na mafundisho ya uwongo!
Wengi wamepoteza hisia zao za uharaka na matumaini katika Ujio
wa Pili wa Kristo. Kuzorota kwa sasa kwa ulimwengu unaotuzunguka kunapaswa
kutuamsha tuone uharaka huo. Mara tatu katika Ufunuo 22, Yesu alionyesha kwamba
anakuja upesi. Tuishi kwa hisia hiyo ya uharaka. Anguka chini ya msalaba na
umruhusu Mungu akuandae kwa ujio wa pili wa Yesu Kristo.
Sisi ni waliosalia wa kanisa la Mungu, si tu dhehebu jingine.
Tumeitwa kumwinua Kristo kwa kuhubiri jumbe hizo za malaika watatu—kuwageuza
watu warudi kwenye ibada ya kweli ya Mungu. Sisi tuna harakati ya kipekee,
yenye ujumbe wa kipekee kwa utume wa kipekee. Usichanganyikiwe kuhusu Ujumbe
maalum wa Mungu. Ngoja nizungumze na Viongozi wote wa Union na konferensi zetu
(139 kati yao), nyinyi ndio wenyeviti wa taasisi zetu za elimu. Jihadharini na
yale yanayofundishwa katika taasisi hizo, hasa madarasa yetu ya dini.
Tunahitaji kurekebisha na kuzitia nguvu upya taasisi zetu.
Shutuma za Uongo kuhusu Uhusiano wa Kanisa na Ekumeni.*
Kanisa la SDA halihusiki katika harakati za uekumene (Umoja wa
makanisa ya Jumapili)na mashirika au mienendo mingine ya kidini. Tunaamini
katika kufanya urafiki na vikundi vingine vya kidini. Ninakutana na viongozi na
viongozi wengi na kujaribu kuwa [karibu] kila mara kwa maombi na viongozi hawa
wa umma tu.
Kanisa limejengwa juu ya mfumo wa uwakilishi unaoongozwa na Roho
Mtakatifu, na tunafanya maamuzi ya moja kwa moja katika chumba hiki. Maamuzi ya
kanisa yanapofanywa katika ngazi ya dunia nzima juu ya maagizo ya Biblia na
Roho ya unabii na kuongozwa na maombi, maoni binafsi yanapaswa kuwekwa kando.
Wakati watu na taasisi zinaasi dhidi ya maamuzi ya pamoja ya kanisa, GC haiwezi
tu kuwafukuza watu kazi au kufuta mashirika bila kupitia mchakato. GC sio eneo
lenye mpangilio wa amri na udhibiti wa watu. Kuna hatua za kinidhamu hizo
zinaweza kutumika lakini kanisa linafanya kazi ya kuwarudisha watu kwenye
umoja. Biblia na Roho ya unabii zimejaa mwongozo kwamba tunapaswa kukubali
maamuzi ambayo hufanywa na kanisa la ulimwengu katika vipindi maalum.
[Tunapaswa kutumia zana tuliyounda kutatua matatizo haya.]
Kutoelewa Kuhusu Roho ya Unabii.*
Kuna mashambulizi ya mara kwa mara kwenye Roho ya unabii, ambayo
mwandishi EGW alitabiri katika maandishi yake. Yasome na yafuate maagizo yake.
Inua utakatifu na kitakasa Sabato ya siku ya saba.
Shiriki imani yako kwa kila njia iwezekanavyo. Kataa mbinu ya
Walaodikia ya kutofanya lolote.
Imetafsiriwa na Pr Gibson MUJUNI Wilson ±255789982615
No comments:
Post a Comment